QJay aomba sapoti yako kwa kazi anayoifanya hivi sasa

 
 
 
Aliekuwa msanii wa nyimbo za bongo fleva "QJay" na kuamua kuachana na mziki huo kwa kuwa ameamua kumrudia mungu "ameokoka" anamba sapoti yako kwa kazi anayoifanya hivi sasa.
 
QJay ambae kwa sasa anafanya kazi aliyokuwa akiifanya mwanzo kabla ya kuanza muziki ambayo ni kutengeneza vifaa vinavyohusisha chuma kama vitanda, mageti na madirisha anaomba sapoti yenu kwa kununua kazi zake kwa dizaini yoyote unayoitaka na anapatikana maeneo ya Mbezi Makonde
 
 "ndio ujuzi ambao nilikuwa nao kabla sijafahamika katika music, ndio kazi ambayo naifanya, kwahiyo kama kuna watu wanahitaji vitu vya namna hiyo vya chuma kwa mfano mageti, madirisha vitanda any disgn ambayo inahusika na chuma wanaweza wakaniona, niko maeneo ya mbezi makonde kama unashuka barabara ya kwenda NSSF, karibu na nyumba za NSSF maeneo ya mkonde makonde chini kule" amesema 
 
QJay pia amedai kutokuhitaji loyalty yoyote ile inayotokana na kazi za muziki aliowahi kuufanya mwanzo ikiwa ni pamoja na ringtones na kuwa muziki wa gospal ataufanya pale tu atakapo kuwa na uelewa mzuri wa dini yake na mambo yanayoizunguka dini yake ila kwasasa amerudia kazi yake hiyo ya mwanzo