Katika hali isiyo ya kawaida mzee mwenye
 umri wa miaka 80 ameomba msaada wa serikali kuingilia kati na kuzuia 
mtoto wake kuuza shamba lake ambalo alilichimba zaidi ya miaka 35 
iliyopita.
Shamba lenyewe lipo Mathira Kenya ambapo mzee analalamika kwamba 
mtoto wake wa kiume amekuwa akiuza sehemu ya shamba hilo kidogo kidogo.
Amesema tofauti na matarajio yake alikuwa akiamini Mtoto huyo 
angekuja kumsaidia uzeeni lakini ndio amekuwa akiuza shamba hilo bila 
ruhusa yake na kuhofia kuwa anaweza kuuza hata kipande cha shamba 
ambacho amechijimbia kaburi lake.

