Mkurugenzi wa chuo chuo cha uandishi habari na utangazaji
Arusha bwana Joseph Mayagila amefungua semina ya siku tatu ya ujasiriamali leo
itakayomalizika siku ya ijumaa chuoni hapo.
pichani ni; Mkurugenzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha Bw. Joseph Mayagila
Bwana Joseph Mayagila amesema kuwa semina hiyo ni muhimu
sana kwa wanafunzi wote kwa sababu dunia ya sasa imejengeka katika misingi ya
ujasiriamali.
Alisema kuwa ili mtu yeyote afanikiwe kibiashara ni lazima
ajue kupanda mbegu, thamani ya muda pamoja na mavuno ambayo ni matokeo ya
kupanda mbegu.
“Unaweza kuhangaika sana kwa lengo la kupata fedha mbegu, kwa kuwa mbegu hizo zitazalisha
fedha nyingi zaidi kupitia mbegu hiyo”
Semina hiyo iliyowahusisha wanafunzi wa kozi zote chuoni
hapo ikiwemo kozi ya uandishi wa habari,
ualimu,sekretari pamoja na kozi ya kompyuta.
picha; baadhi ya wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wakiwa kwenye semina leo
Katika semina hiyo ziliawasilishwa mada kuu tatu na
wakufunzi wa chuo hicho, ambapo mwalimu Onesmo Elia Mbise aliwasilisha mada ya
mikakati ya kibiashara, na mada ya
huduma kwa wateja iliwasilishwa na bw, Christian Ndege na mada ya Miongozo ya
mjasiriamali, iliwasilishwa na Mratibu wa kitengo cha ujasiriamali chuoni hapo bw,
Adrea Ngobole.
Bwana Maygila alisema kuna kuuuza na kununua lakini sio kila
mtu anaweza kuuza na kuwataka wote kujenga fikra zao katika kuuza ila waweze
kujenga maisha yao
Alisema kama mtu antaka kufanikiwa maishani na kutaka
kununua vitu vya thamani ni lazima mtu ajipange vizuri katika kuuza
“Duniani kuna kuuza na kununua huwezi kukwepa kununua lakini
sio kila mtu anaweza kuuza, unaweza
kuuza mawazo, jambo na bidhaa” Alisema Mayagila
Mayagila aliwashauri wanafunzi wake kujiunga kwenye taasisi za kifedha kwani mkopo ni
fedha mbegu na zitawasaidia kufanikisha
biashara zao na kuzaa zaidi
Alihitimisha ufunguzi wa
semina hiyo kwa kusema kwamba ili mtu yeyote afanikiwe ni lazima kusoma
vitabu mbalimbali
“Nyumba isiyyo na vitabu ni mfu, akili isiyopenda kusoma ni
mfu pia ,ili uweze kufanikiwa nilazima ulipe gharama za kufanikiwa”
Katika semina hiyo ziliawasilishwa mada kuu tatu na wakufunzi wa chuo hicho, ambapo mwalimu Onesmo Elia Mbise aliwasilisha mada ya mikakati ya kibiashara, na mada ya huduma kwa wateja iliwasilishwa na bw, Christian Ndege na mada ya Miongozo ya mjasiriamali, iliwasilishwa na Mratibu wa kitengo cha ujasiriamali chuoni hapo bw, Adrea Ngobole.
Baadhi ya wakufunzi waliongoza semina;wa kwanza kushoto juu ni Bw. Christian Ndege akifuatiwa na Bw. Onesmo Mbise, Picha kubwa chini ni Bw.Andrea Nobole
Mwandishi;Benson Mremi
Mhariri;Ckephas ilan