Tue Nov 25 2014

Spika wa Bunge ANNE MAKINDA
Akijibu mwongozo bungeni Mjini DODOMA Spika MAKINDA amesema kwa mujibu wa taratibu za bunge, kamati iliyopewa kazi ya kushughulikia ripoti ya CAG inapaswa kumwandikia Spika barua kumtaarifu kuwa imekamilisha kazi yake, ili muswada huo upate fursa ya kujadiliwa.
Kwa mujibu wa maelezo ya Spika, anachosubiri sasa ni taarifa ya kamati kama imekamilisha kazi hiyo ili aweze kuipanga kujadiliwa.
Katika hatua nyingine Waziri wa Fedha SAADA MKUYA amewasilisha bungeni muswada wa sheria ya kodi ya ongezeko la thamani wa mwaka 2014