MESSI ADOKEZA KUHAMA BARCELONA

 
MESSI-SIMANZI
LICHA ya kusema kuwa anataka abaki Barcelona milele lakini Lionel Messi ameacha mlango wazi kuihama baada kudokeza upo uwezekano wa kuhama baada ya Msimu huu.
 
Messi, ambae sasa ni Nahodha wa Argentina na ambae amewahi kuwa Mchezaji Bora Duniani mara 4, alijiunga na Chuo cha Soka cha Barca akiwa na Miaka 13 na kudumu hapo hadi sasa.

Lakini Messi, mwenye Miaka 27 sasa, amekuwa na kiwango hafifu kwa kipindi cha Miezi 18 akikumbwa majeruhi ya mara kwa mara na pia kupatwa na misukosuko ya kuburuzwa Mahakamani yeye na Baba yake Mzazi huko Spain akidaiwa kukwepa kulipa Kodi.

Akiongea na Jarida la Nchini kwao Argentina, Olé, Messi alikaririwa:
 “Kwa sasa bado nipo Barca na nina malengo kutwaa Mataji lakini baada ya hapo tuaona. Vitu vinaweza kubadilika sana na haraka kwenye Soka. Ingawa Siku zote nimesema napenda kubaki Barca milele lakini mara nyingine vitu haviendi unavyotaka.”

Msimu uliopita Barca ilitoka kapa bila kutwaa Taji kubwa na Msimu huu wapo Nafasi ya Pili kwenye La Liga wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Real Madrid baada ya Mechi 11 za Ligi.

Kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI, Barca wameshafuzu kuingia Raundi ya Mtoano ya Tumu 16 huku wakiwa na Mechi 2 za Kundi lao mkononi.

Ikiwa Messi atapelekwa Sokoni kuuzwa basi Dau lake linakadiriwa litakuwa si chini ya Euro Milioni 100