ROONEY ACHEZA MECHI YA 100 ENGLAND IKISHINDA 3-1

ROONEY-BUTI-NIKE100
NAHODHA Wayne Rooney jana ktka Uwanjani Wembley amecheza Mechi yake ya 100 wa England na pia kuwanasua toka Goli 1 nyuma na kusawazisha walipocheza na Slovenia Mechi ya Kundi E na hatimae kushinda Bao 3-1.
 
Kabla ya Mechi kuanza, Rooney alikabidhiwa Kofia ya Dhahabu na Sir Bobby Charlton ikiwa ni Tuzo kwa kuichezea England Mechi 100.

Hadi Mapumziko, Bao zilikuwa 0-0.

Kipindi cha Pili Dakika ya 57 Jordan Henderson alijifunga mwenyewe kwa Kichwa kufuatia Frikiki na kuwapa Slovenia uongozi lakini Dakika 2 baadae Rooney aliisawazishia England kwa Penati baada ya yeye mwenyewe kukwatuliwa na Bostjan Cesar.

Danny Welbeck alifunga Bao 2, Dakika za 66 na 72, na kuipa England ushindi wa Bao 3-1.
Ushindi huu umeifanya England ipae kileleni ikiwa na Pointi 12 ikifuatiwa na Lithuania na Slovenia zenye Pointi 6 kila moja.