WIMBO WA YAMOTO NA CHRISTIAN BELLA WAVUJA KABLA HAUJAKAMILIKA

WIMBO WA YAMOTO NA CHRISTIAN BELLA WAVUJA KABLA HAUJAKAMILIKA …watu watumiana kwa Whatsapp kama hawana akili nzuri 
 

Wimbo mpya kabisa wa Yomoto Band ambao ndani yake ameshirikishwa mkali wa masauti Christian Bella, umevuja kabla hata haujakamilika na tayari umesambaa kinoma kwa wadau wa muziki.

Hata kabla haujafanyiwa mixing na kupekekwa radioni, wimbo huo ukavuja na katika hali isiyotarajiwa na bila kujali ubora wa kazi, mashabiki wakaanza kutumiana wimbo huo kwenye simu zao kupitia mtandao wa Whatsapp na kuenea kila kona hadi kwa watu wa bodaboda.

Ngoma hiyo iliyopewa jina la “Rubani wa Moyo” inatisha kwa utamu, imejaa mistari mitamu ya mapenzi huku Bella na madogo wa Yamoto wakifunikana ile mbaya kwenye kutuma masauti.