Prof MUSSA JUMA ASSAD
Prof ASSAD ameeleza hayo mjini ARUSHA baada ya kufungua Mkutano wa Bodi ya wahasibu NBAA ambapo amesema katika ripoti hiyo ya TEGETA ESCROW kuna mambo machache yanayohitaji kufanyiwa kazi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya NBAA, Profesa ISSAYA JAILO, amesema wahasibu na wakaguzi wakuu wa hesabu ni vema wakafahamu umuhimu wa masuala ya mafuta ,gesi pamoja na utalii ambayo ndiyo chanzo cha uchumi mkubwa kwa Taifa, huku Taasisi na mashirika yaliyofanya vizuri katika hesabu zake yakazawadiwa tuzo mbalimbali

