CHELSEA YAENDELEZA USHINDI,MAN CITY NA ARSENAL NAZO ZASHINNDA

VINARA wa Ligi Kuu England, Chelsea, Jumatano Usiku wameichapa Tottenham Bao 3-0 na kuendelea kupaa kileleni mwa Ligi hiyo.

 Bao za Chelsea zilifungwa na Eden Hazard, Didier Drogba na Loic Remy. 
   
Nao Arsenal wameitungua  Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 89 la Alexis Sanchez.

Mabingwa Watetezi Man City wameichapa Sunderland Bao 4-1 kwa Bao za mbili za Sergio Aguero, Jovetic na Zabaleta huku Bao la Sunderland likifungwa na Wickham.

Everton na Hull City zilitoka Sare ya Bao 1-1 wakati Romelu Lukaku alipotangulia kuifungia Everton na Sone Aluko kuisawazishia Hull Hull City.