GERRARD AIPA USHINDI LIVERPOOL



Baada ya mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha katika michuano ya ndani na nje ya nchi yao – klabu ya Liverpool leo imejitupa uwanjani kucheza na timu iliyowapa kipigo kizito Man United – klabu ya Leicester City.

Mchezo huo wa Barclays Premier League uliochezwa katika dimba la Leicester City umemalizika kwa Liverpool kuwatafuna Leicester 3-1.


Magoli ya Adam Lallana, Steven Gerrard na Jordan Henderson yalitosha kuwapa pointi 3 Liverpool na kuwafanya sasa kutimiza pointi 20 katika msimamo wa ligi kuu ya England