DIEGO COSTA KUPINGA SHITAKA LA FA


STRAIKA wa Chelsea Diego Costa ambae alifunguliwa Mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kwa Kosa la Mchezo wa Vurugu kufuatia kumkanyaga Beki wa Liverpool Emre Can kwenye Mechi ya Marudiano ya Nusu Fainali ya Capital One Cup dhidi ya Liverpool Jumanne Usiku, ameamua kupinga Mashitaka hayo.
Kwenye Mechi hiyo ambayo Chelsea waliifunga Liverpool 1-0 na kutinga Fainali, Costa ameshitakiwa kwa kumtimba kwa makusudi Beki wa Liverpool Emre Can katika Dakika ya 12 ya Mechi hiyo.
Costa anatarajiwa kulikabili Jopo Huru la Watu Watatu la FA Ijumaa Asubuhi na ikiwa Kamisheni hiyo itamsafisha basi atakuwa ruksa Jumamosi kuwakabili Mabingwa wa England, Manchester City, Uwanjani Stamford Bridge kwenye Mechi ya Ligi Kuu England inayozikutanisha Timu za Kwanza na za Pili huku Chelsea wakiwa mbele kwa Pointi 5
Ikiwa Jopo hilo litampta na hatia, Costa atafungiwa Mechi 3 kuanzia hiyo na Man City na nyingine ni zile dhidi ya Aston Villa na Everton.