
Figo ametangaza azma hiyo akitumia ukurasa wake binafsi wa mtandao wa kijamii wa Twitter ambapo aliueleza ulimwengu lengo lake la kuingia kwenye kinyang’anyiro hicho kinachomhusisha rais wa sasa Sepp Blatter .
Figo anakuwa mgombea wa sita kutangaza azma ya kuwania urais wa FIFA baada ya Blatter mwenyewe , mchezaji mwingine wa zamani David Ginola , makamu wa rais wa FIFA
ambaye pia ni rais wa chama cha soka cha Jordan Prince Ali Bin Al
Hussein , rais wa chama cha soka cha Uholanzi Michel Van Praag , na
kiongozi wa zamani wa FIFA Jerome Champagne .

igo amesema kuwa sababu inayomuongoza
kuingia kwenye mbio hizo ni kuleta mabadiliko ndani ya shirikisho hilo
na kupunguza kashfa zinazoendelea kulikumba shirikisho hilo .