MAKAMPUNI 11 ACACIA BUZWAGI KUBURUZWA MAHAKAMANI NA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA


HALMASHAURI ya Mji wa Kahama Mkoani Shinyanga imedhamiria kuyafikisha Mahakamani Makampuni 11 yanayofanya kazi katika Mgodi wa Acacia Buzwagi kwa kosa la kukaidi  kulipa kodi ya huduma ( Service leav) katika Halmashauri hiyo.
Hayo yamebainika jana katika kikao cha baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Kahama baada ya  madiwani kutaka kujua mapato na matumizi ya Halmashauri kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita ikiwa ni sambamba na kujua kama makampuni hayo yamelipa kodi hiyo ya huduma .
Akitolea ufafanuzi suala hilo Mweka hazina wa Halmashauri hiyo Wilfred Kishere amesema kuwa kuna baadhi ya makampuni yamekuwa yakikaidi kukaguliwa kwa lengo la kuona faida wanayoipata hali ambayo inaleta ugumu kukadiria aslimia 0.3  ya faida wanayoipata ili kuweza kuilipa Halmashjauri husika.
Kishere aliyataja Makampuni hayo kuwa ni pamoja na  Mafinga Best, Shimiyu Constraction, Isamilo Supplies, Gorden Valley Hotel, G4S security Services, Fresters Investment Company Limited,  Beb Company Limited, Agreco Project , AGB Eqipment pamoja na Kasekdindis Contraction.
Sambamba na hayo madiwani hao wametoa masikitiko yao kwa watumishi wa Halmashauri ya mji wa Kahama kuwa pamoja na kuwa na vyanzo vingi vya mapato wamekuwa mazembe katika kukusanya mapato ya ndani.
Mmoja wa Madiwani hao Aoko Nyangusu amesema kuwa watumushi wa Halmashuri hiyo wamekuwa wakikaa ofisini bila ya kukusanya mapato huku akisisitiza kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara hawana leseni za kufanya shughuli hizo.
Aidha Diwani huyo alisema kuwa Halmashauri hiyo imekuwa haifikii malengo ya kukusanya mapato ya ndani kutokana na uzembe unaofanywa na wahasibu hao kwa kutokukusanya mapato hali ambayo halmashuri imekuwa haina fedha za kutosha hata za kuwalipa wakandarasi wanaoidai.