MWANAMKE ACHARANGWA MAPANGA HADI KUFA KAHAMA KISA WIVU WA MAPENZI.



Mwanamke mmoja Schorastica  Shija (55) mkazi wa Mtaa wa Kitwana kata ya Busoka wilayani Kahama mkoani Shinyanga ameuawa kwa kukatwa kwa mapanga kichwani  na watu wasiojulikana kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa Kimapenzi.

Akizungumza na suala hilo afisa mtendaji wa Mataa huo, Rafael Jumanne alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa tano usiku wakati  Scholastica shija akiwa  numbani kwake anajiandaa kulala akiwa na wajukuu zake wawili.

Alisema baada ya majambazi hayyo ambao idadi yao haikufahamiaka, walianza kumcharanga mapanga kichwani na  mkono wa kulia hali ambayo ilisababisha kuvuja kwa damu nyingi na baadaye kifariki dunia.

“Nilipigiwa simu majira ya saa tano usuku na mwenyekiti wangu wa Mtaa na baada ya kufika  eneo la tukio nilikuta  tayari  ameshaaga dunia  huku damu nyingi zikiwa zinaendelea kuvuja kwa wingi”.alisema Jumanne.

Afisa Mtendaji huyo alisema   chanzo cha  mauji hayo bado haijafahamika ingawa zinahusishwa na wivu  wa kimapenzi na kwamba   jeshi la Polisi lilifika eneo la Tukio na kuupeleka mwili wa maraehemu katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya ya Kahama.

Alisema Mbali na maujai hayo, pia baiskeli moja aliibiwa  na  majambazi hayo  huku hakuna  mtu yeyote ambaye alikamatwa kuhusiana na tukio hilo na kwamba watashirikiana na jeshinla Polisi kufanya upelelezi.

Akizumgumza kwa nja ya Simu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shimyanga Justus Kamugisha  alidhibitisha kutokea kwa tukio  hilo na hakuana anayeshikiliwa huku upelelezi unaendelea kufanyika ili kuwabaini na hatimaye kuwafikisha  katika sheria.

Kamanda kamugisha aliwataka wananchi kuacha kuamini imani za Kishirikia ambazo kimsingi   zinaleta uchochezi wa mauaji ya vikongwe huku akiitaka jamii ishirikiane na jeshi la Polisi kuwafichua.