SERIKALI WILAYANI KAHAMA YAPIGA MARUFUKU WANANCHI KUTUMIA MAJI YA VISIMA,BAADA YA KAMPUNI YA ACACIA KUSAMBAZA MABOMBA YA MAJI.


MKUU WA WILAYA YA KAHAMA BENSON MPESYA.

SERIKALI wilayani Kahama mkoani Shinyanga imepiga marufuku wananchi wa kijiji cha namba tisa kata ya Bulyanhulu wlayani hapa kutumia maji ya visima pamoja na kuendesha shughuli za kilimo kufuatia kuvuja kwa bwawa la maji ya mgodi wa Dhahabu wa ACACIA Bulyanhulu yanayosadikiwa kuwa na sumu ya Syned.

Akizungumza na wandishi wa Habari mkuu wa wilaya ya Kahama,Benson Mpesya alisema serikali imeamua kupiga marufuku utumiaji wa visima vya maji pamoja na shughuli za kilimo katika kijiji hicho mpaka mpaka baraza la Usimamizi wa mazingira(NEMC) itakapomaliza uchunguzi kuhusu kemikali hizo.

Mpesya alisema kufuatia bwawa hilo kujaa maji na kutiririka katika kijiji hicho kilichopo jirani na mgodi huo uongozi wa kampuni ya ACACIA iliamua kufunga mabomba sita ya maji kutoka katika mgodi huo kwenda kwenye kijiji hicho huku kwa lengo la kuwasaidia wananchi mpaka hapo uchunguzi utakapokamilika.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa bwawa hilo lilianza kutiririsha maji hayo tangu tarehe 9/01/2015 kufuatia mvua kubwa ya mawe iliyonyesha yenye milimita 50 na hivyo kusababisha bwawa hilo kufurika na maji yake kuelekea katika kijiji jirani cha namba tisa.

Hata hivo Mpesya alisema kijiji hicho ambacho kipo ndani ya leseni ya mwekezaji wa kampuni ya hiyo ambapo bado haijalipa wananchi fidia kilikuwa na jumlaya kaya tatu zenye watu wapatao 27 huku madhara yaliyotokea ni kukauka kwa mazao na maji kubadirika rangi tofauti na yalivyokuwa hapo awali.

Mpesya alisema kufuatia hali hiyo kampuni ya ACACIA ilamua kuwapeleka Jumla ya wananchi 138 katika hospiatli ya wilaya ya Kahama kwa uchunguzi huku matokeo ya vipimo yakionyesha hakuna aliyeathirika na madawa hayo mbali ya kukutwa na magonjwa mengine ya kawaida.

Pia Mpesya alisema ameunda kamati ya kuangalia hasara zilizotokea kwa wananchi na kama ni mazao au watu zitaonekana mgodi huo utawalipa fidia wananchi hao ili kuendelea kuwa namahusiano mazuri baina ya mwekezaji na wananchi wanaoishi jirani na mgodi huo.

Kwa upande wake Afisa usalama wa mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu Abdallah Mssika akiongea kwa niaba ya msemaji wa mgodi huo alisema  kufuatia kutokea kwa tukio hilo uongozi umeimarisha miundombinu ya visima na kwamba hali hiyo haiwezikujirudia tena.

Alisema mabwawa yamekarabatiwa katika kiwango cha hali ya juu na kuongeza kuwa mabomba hayo sita waliyoyapeleka katika kijiji hicho ni ya kudumu hivyo wananchi hawatatumia maji ya visima tena kama siku za nyuma huku wakisubiri ripoti ya NEMC kutoa majibu sahihi juu ya uchunguzi kemikali hizo. 

                                    Credit;kijukuu cha bibi k blog