WANAFUNZI ZAIDI YA 1200 KATIKA SHULE ZA KILIMA A NA B MJINI KAHAMA WANAKAA CHINI.

 
PICHA HII SI UASILIA WA HALI YA KILIMA.

Zaidi ya wanafunzi 1200 katika shule za msingi Kilima A, na B, Kata ya Nyihogo halimshauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga  wanakaa chini kutokana na shule hizo kuwa na uhaba wa madawati kwa muda mrefu licha ya  kuwa katikakati ya mji.

Hali hiyo ilibainika wakati wa ziara ya baadhi ya viongozi wa Kata ya Nyihogo kufika shuleni hapo  kujionea hali ya miundombinu iliyopo na kukuta  idadi kubwa ya wanafunzi wakikaa chini  kwa zamu.

Akizugumzia hali hiyo Mwalimu  Mkuu wa Shule Msingi Kilima A, Francisca Kisaka alisema shule hiyo inajuma ya wanafunzi 1200, Madawati 100 ambapo wanaokalia madawati ni wanafunzi 300 pekee huku wanafunzi 900 wakiwa wanakaa chinikwenye sakafu.

Alisema   kutokana na ukosefu wa madawati, baadhi ya madarasa yamekuwa hayatumiki na badala yake yanatumika katika kuhifadhi kuni huku shule hiyo ikikosa pia choo cha walimu hali ambayo inawalazimu kutumia vyoo vya wanafunzi.

Naye mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kilima B, Restiel Mlay alisema shule hiyo inajumla ya wanafunzi 1165,ambapo  wanaokaa chini ni zaidi ya 300, kutokana na shule hiyo kuwa na ukosefu wa madawati 107.

Alisema shule hiyo pia inakabiliwa na  uharibifu wa   milango  mablimbali  hasa katika vyoo kutokana na kuwepo kwa vijana wanaotumia eneo hilo kuvuta bangi  na uhalifu mwingine, huku jamii inayozunguka eneo hilo kutumia vyoo vya shule kujisaidia.

Hata hivyo shule hizo mbili zinakabiliwa na ukosefu wa nyumba za walimu,  pamoja na Ofisi ya walimu hali ambayo wanatumia ofisi moja  na wakuu wa shule hivyo  serikali inapaswa kufanya juhudi za makududi kukalibilana na changamito hizo.

Diwani wa Kata ya ya Nyihogo Amos Spemba aliitupia lawama  kamati ya shule hizo kwa kushindwa kuweka mpango kazi madhubuti ya kutatua kero hizo  na kwamba ameahidi kulifanyia kazi na hatimaye kwa kulifikisha katika halamshauri husika.

Afisa mtendaji wa mtaa wa huo Simon Mabumba aliwataka walimu wakuu kukaa  na kamati ya shule na kufanya kikao na wazazi ili kuwashirikisha kuchangia maendeleo ya shule, jambo ambali liliungwa mkono na Mratibu elimu wa Kata hiyo  Winifrida Madata. 

                                                                credit;kijukuu cha bibi k blog