JURGEN KLOOP NA XAVI WAAGWA KWA HESHIMA KUBWA NA MASHABIKI WAO

"DANKE JURGEN", YAANI AHSANTE JURGEN. HIVI NDIVYO MASHABIKI WA DORTMUND WALIVYOMUAGA KOCHA WAO MWENYE MAFANIKIO MAKUBWA, JURGEN KLOOP AMBAYE AMEAMUA KUONDOKA MWENYE KWA HIARI YAKE NA KUMPA MTU MWINGINE NAFASI YA KUENDELEA KUINOA TIMU HIYO.





Picha,Barcelona na mashabiki wake walivyomuaga Xavi.

Wachezaji wa timu ya Barcelona wamevalia jezi maalum katika mechi yao ya mwisho ya msimu huu ili kutoa heshima kwa kiungo wao wa kati Xavi ambaye anakamilisha uhusiano wake wa miaka 24 na klabu hiyo . 
 
Xavi amepewa kwaheri maalum katika mechi dhidi ya Deportivo la Coruna iliyochezwa katika uwanja wa Nou Camp siku ya jumamosi.

Xavi mwenye umri wa miaka 35 ambaye amejishindia medali yake ya nane ya la liga alitangaza siku ya alhamisi kwamba ataondoka Barcelona mwishoni mwa msimu huu ili kujiunga na kilabu ya Qatar Al Saad. Xavi alisema uamuzi huo umekuwa mgumu kwake.
_83185762_xavi_fcbarcelona _83192343_xavilaligatrophygetty3 xavigetty1 xavilaligatrophygetty1 xavishirtgetty1 xaviwavesgetty2
zavi   8 zavi 6 zavi 7