WIZ KHALIFA AMETANGAZA ALBAM YAKE MPYA ‘Rolling Papers 2: The Weed Album’.

wiz
Akiwa anaendelea kupata mafanikio na wimbo wake mpya wa “See You Again” ukiwa umeshikilia namba moja kwenye chati za bilboard kwa wiki ya sita sasa rapa Wiz Khalifa ametangaza rasmi ujio wa album mpya.

Mmiliki huyu wa Taylor Gang ametumia twitter kusema kuwa album itaitwa Rolling Papers 2: The Weed Album,ambayo ni muendelezo wa album yake ya mwaka 2011 Rolling Papers, iliyokuwa na wimbo kama “Black and Yellow.”

Rolling Papers 2 inakuja baada ya album ya mwaka 2014 Blacc Hollywood, iliyoshika namba moja kwa kuuza kopi 90,000 ndani ya wiki ya kwanza